"Huwezi kuamini, watu wameiba Mahakamani" - RPC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za wizi baada ya kuvunja Mahakama ya Wilaya ya Njombe na kuiba vitu mbalimbali vya ofisi hiyo ikiwemo Laptop tatu (3) na Sukari kiasi cha Kg 25, waliokamatwa yupo aliyeiba na mwingine aliyeenda kuuziwa Laptop hizo.


Taarifa hiyo imetolewa hii leo Septemba 7, 2020, na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Hamis Issah na kuongeza kuwa tukio hilo ni la ajabu na hivyo wanangoja utaratibu ukamilike tu ili waweze kuwafikisha mahakamani kwa kuiibia Mahakama.

"Huwezi ukaamini na ninaomba uamini, kuna watu wameenda wamevunja Mahakama ya Wilaya ya Njombe, hivi ninavyoongea hapa Mahakama hiyo ilivunjwa, ikaibiwa vitu mbalimbali ikiwemo Sukari Kg 25, na Laptop 3, tumeweza kukamata hizo Laptop na watu wawili tumewakamata, yaani watu walivyo majasiri hawaogopi hata vyombo ambavyo vinawatendea haki", amesema Kamanda Issah.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad