Jinsi familia tatu za Kenya zilivyotawala siasa za Kenya, je kutakuwa na mabadiliko?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Siasa za nchi ya Kenya-kwa miaka mingi tangu Kenya kupata uhuru wake mwaka wa 1963 - zimekuwa zikizunguka sifa na taswira ya familia mbili- familia ya Kenyatta na ile ya Odinga.



Daniel arap Moi, aliyekuwa rais wa pili wa Kenya, alikuwa rais aliyekaa mamlakani kwa muda mrefu zaidi - miaka 24, na rais wa tatu, Mwai Kibaki ambaye alikuwa mamlakani kati ya 2002-2013, lakini unapofuatilia hisia na siasa za Kenya, taswira inayotawala ni kati ya familia mbili-ile ya Kenyatta na ile ya Odinga.




Ikumbukwe kwamba Mzee Jomo Kenyatta na Jaramogi Oginga Odinga walianza kutawala siasa za Kenya hata kabla ya nchi ya Kenya kupata uhuru. Wawili hawa walikuwa viongozi shupavu wa jamii zao- Kenyatta akiiongoza jamii ya Agikuyu na Odinga akiongoza jamii ya Luo.




Wanasiasa hawa wawili walifanya kazi kwa bidii bila woga kuwezesha jamii zao na kuzikinga dhidi ya unyanyasaji wa wakoloni huku wakiwa wamependwa na kutajika katika jamii zao kama viongozi shupavu na wakombazi.




Mzee Jomo Kenyatta na Jaramogi Oginga Odinga walikuwa mashuhuri nchini Kenya katika harakati na mapambano ya kupigania uhuru wa Kenya na walivutia uungwaji mkono kutoka kwa viongozi wengine mashuhuri nchini Kenya katika harakati za ukombozi.




Hata hivyo, mambo yalibadilika baada ya uhuru. Katika kitabu chake, Not yet Uhuru, Odinga anaeleza kuwa kwa Wakenya wengi, uhuru ulikuwa bado haujapatikana kwa sababu mkoloni mpya alikuwa amechukua nafasi ya mwingine.




Kilichofuatia baada ya uhuru ni kujiuzulu kwa Odinga kutoka serikali ya Kenyatta na hatua za kisiasa zilizofuata zilikuwa ni mabishano makali ya kihistoria baina ya familia hizi mbili mashuhuri nchini Kenya kwa miongo takriban mitano.




Miaka miwili kabla ya kifo cha rais wa kwanza wa Kenya, Jomo Kenyatta, mnamo Agosti 1978, na baada ya uchaguzi uliokuwa na ushindani mkali wa mwaka wa 1974, kinyang'anyiro kilifikia kilele, huku washidani wakibishana na kutupiana maneno kwenye mikutano ya hadhara kuwaonya wananchi wa Kenya dhidi ya hatari za uwezekano wa Daniel arap Moi kumrithi Jomo Kenyatta.




Kikundi hiki kilitaka katiba kubadilishwa ili makamu wa rais asiwe na uwezo wa kumrithi rais iwapo rais atakufa, mabadiliko ambayo hayangemruhusu Moi kumrithi Jomo Kenyatta.




Moi alitoka kabila la Wakalenjin kutoka Baringo na kikundi kilichofahamika kama "Kiambu Mafia" kilimdharau na hakikuweza kuwaza uwezekano wa Moi kuwa rais wa Kenya.




Baada ya hapo, yeye pamoja na mtoto wake, Raila, walishutumiwa kwa makosa ya kila aina, kutupwa kuzuizini, kuzuiliwa nyumbani, na kuzuiliwa kuzungumza kwenye hadhara ama kuandaa mikutano na shutuma nyingine nyingi zikiwafuata.




Hatimaye, Jomo Kenyatta alimteua Daniel arap Moi kuwa makamu wake na kuonyesha ni nani aliyemtaka kama mrithi. Moi, aliyetoka kwenye jamii iliyoonekana ndogo- Kalenjin- wakati huo, alionekana kama chaguo zuri na kama ngazi ya kuleta jamii pamoja baina ya makundi mbali mbali.




Uhusiano baina ya faimilia ya Odinga na ile ya Kenyatta haukuweza kuwa mzuri kisiasa.




Baada ya Daniel Moi kuchukua hatamu za uongozi aliendeleza sera za Mzee Kenyatta kisiasa na kuitenga familia ya Odinga.




Raila Odinga na babake, Jaramogi, walitajwa kwenye jaribio la kuipindua serikali ya Kenya lililofanyika mwaka wa 1982 ambalo halikufaulu.




Raila alizuiliwa kwa miaka sita bila kufikishwa mahakamani lakini aliachiliwa mwaka wa 1989.




Hata hivyo, Raila alifungwa tena karibu mwaka mmoja baadaye, wakati huu, pamoja na wakereketwa wengine wa kupigania mfumo wa vyama vingine kama vile Kenneth Matiba na Charles Rubia.




Baada ya kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini Kenya, Raila Odinga alirudi Kenya na kujiunga na Forum for the Restoration of Democracy (FORD, wakati huo ikiongozwa na babake, Oginga Odinga).




Kilichofuata baadaye ni msururu wa kushirikiana kwa vyama, miungano, na kuundwa kwa vyama vipya.




Wakati mmoja, kwa mshangao mkubwa, Raila aliungana na Moi na kuunda chama kipya kilichojulikana kama New Kanu. Hali hii ilipelekea baadhi ya wandani wake, wapinzani na wafuasi sugu kumuita mtu ambaye yuko tayari "kulala na shetani" ili kufikia lengo lake la kuwa rais wa Kenya.




Alifanya kazi kama waziri wa kawi katika serikali ya mwisho ya Moi.




Kinachobainika katika historia ya siasa za Kenya, wakati wa hatamu za uongozi wa Moi, familia ya Kenyatta haikujishughulisha na siasa; badala yake ilizingatia shughuli za kuunda mtandao wa biashara.




Halafu, bila kutarajiwa, Moi alimteua Uhuru Kenyatta kama mrithi wake. Hili lilifanya wanasiasa wengi kuondoka kwenye chama tawala kwa sababu ya kuhisi kwamba Uhuru Kenyatta alikuwa na ujuzi wa kiwango cha chini katika serikali kuchukua nafasi hii.




Baadaye, Uhuru Kenyatta aliwania Urais kama mgombea kwa tiketi ya Kanu katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2002 dhidi ya Mwai Kibaki, ambaye wakati huo aliungwa mkono na Raila Odinga.




Hata ingawa alimfanyia kampeni sana Mwai Kibaki hadi kuchaguliwa kuwa Rais, Odinga aliachwa bila wadhifa wowote jambo ambalo lilimuudhi kisiasa na kuona kama aliyechezewa shere.




Kwa sababu hii, Raila Odinga aliondoka na kuunda muungano wa Orange Democratic Movement (ODM).




Lililoshangaza lilifuata; Uhuru Kenyatta ndiye aliyekuwa anamuunga mkono Kibaki dhidi ya Odinga kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2007.




Mwai Kibaki alitawazwa mshindi kwa tofauti ya kura chache, ushindi ambao ulipingwa na chama cha ODM.




Kufuatia haya, fujo zilizuka nchini Kenya; jijini Nairobi na miji mingine na kupelekea vifo vya zaidi ya Wakenya elfu moja na wizi na uharibifu mkubwa wa mali.




Vita na hali ya wasiwasi ilimalizika kutokana na makubaliano baina ya Raila Odinga na Mwai Kibaki ambapo serikali ya muungano iliundwa mwaka wa 2008 huku Mwai Kibaki akiwa rais na Raila Odinga akiwa Waziri Mkuu.




Uhuru Kenyatta alikuwa mojawapo wa watu walioshtakiwa kwenye mahakama ya kimataifa ya ICC kwa kuchochea michafuko nchini Kenya lakini kesi yake haikuendelea kwa ukosefu wa ushahidi na mashahidi.




Kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2013, Kenyatta, ambaye sasa alikuwa kiongozi wa muungano mpya, Jubilee, alishindana na Raila kwa mara nyingine, (wakishirikiana na William Ruto ambaye walikuwa wameshtakiwa naye kwenye mahakama ya ICC) ambaye pia alikuwa ameunda muungano mkubwa, Coalition For Reform and Democracy (CORD).

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad