Kama Unataka Kufurahia Mapenzi oa Mwanamke Asiye na Kazi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wanawake wasio na Kazi wanakua hawana mambo mengi. Ukitoka kwenye mihangaiko yako anakupokea na kukukaribisha Nyumbani kwa furaha. Utakuta chakula kishaiva, utakuta Watoto wasafi kama mmebahatika kuwa nao, hata ukimuachia hela ya matumizi anatumia Vizuri tena unampa hela kwa furaha kabisa. Mkibahatika kupata Mtoto hutakuwa na mawazo ya Mtoto wako kupigwa na House girl. Ukitembelewa na Familia, hawataboreka kwani muda wote watakua na mwenyeji Mama mwenye Nyumba.

Jidanganye uoe Mwanamke mwenye Kazi. Asilimia kubwa wanarudi wamechoka kiasi kwamba hata mkilala hakugeukii wala hataki umguse. Atataka haki sawa eti akipika wewe ufue Nguo au umsaidie Kupika. Mara chache atakutengea Maji ya kuoga. Muda mwingi anatoka Kazini amenuna, hata akichelewa hataki umuulize alikua wapi.

Wana viburi sana, ukiwauliza kitu wanajibu kwa nyodo, hatakusikiliza. ukimsemesha kidogo tu ataenda kulala kwa marafiki zake au kwa ndugu zake. Haoni aibu kukukolomea Mwanaume hata mbele za watu. Anajifanya anawivu sana, atapiga Simu kila dakika kukuuliza ulipo as if wewe mtoto mdogo hujui pa kwenda.

Anapewa Mshahara lakini hautojua unaenda wapi kwani kila siku utaombwa hela ya Salon. Siku ukiishiwa ukamuomba hela ya Bia hatakupa bali atasema siwezi kukupa hela yangu ukahonge Malaya zako.

Siku akifurahi atakuletea zawadi ya Shati, mara moja kwa Miezi Mitano kana kwamba halipwi Mshahara. Dawasco wakimkuta hatawapa hela yake hata kama anayo, atawambia hayupo.

Ukioa Mwanamke mwenye kazi utamfaidi siku ukiumwa, ataomba ruhusa ili aje akuhudumie, atakununulia sana Socks na Matunda Matunda. akitaka kununua kitu atakua na kianzio sana sana ataomba umuongezee Hela.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

7 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Utajua tuu wanaume wenye mawazo finyu. Mnataka muwaache wake zenu home...mkirudi mmelewa mnawapiga na hamuwapi chochoote zaidi ya
    stress. Na bado ukatafute michepuko inayofanya kazi. Mtawadanganya hao haooo ambao hawajielewi. Mimi baba na mama woote wanafanya kazi na kila mtu anaplay part yake viizuuuriii hayoo yoote unayosema. Mi nadhani ni kujipanga zaidi ya kumuweka mtu ndani ili atombwe na houseboy manake mwenzio ana energy tele...wewe unarudi umechoka.

    ReplyDelete
    Replies
    1. kweli kabisa awadanganye haohao makolo mshenzi mkubwa !

      Delete
  2. Maada ni nzuri sana ila hapo inategemea tu na tabia ya mtu,,,,,,,wawezakuwa na mke asiye na kazi ila bado akakupa stress coz yeye kila siku ni wa vibarazani na wanawake wenzie wasio na kazi kutwa umbea na kutafuta mabwana wengine apate pesa ya saloon,,,,,,vile vile mwanamke mfanyakazi ni mbaya akishindwa kutambua wajibu wake,,,,,lakini mimi nafanya kazi na nnafanya kila lililozuri kwa mume wangu ...

    ReplyDelete
  3. Mwanamke asiye na kazi ni yupi huyo? Kwani kazi za nyumbani sio kazi?
    Labda uoe mke, kisha umuwekee housegirl wa kufanya kazi zote za ndani na kupika. Yeye kazi yake iwe kukaa tu anaangalia TV na kulala ndio ukirudi kutoka kazini utamkuta hajachoka.

    Lakini eti mwanamke yuko nyumbani afanye kazi zote za kusafisha nyumba, vyombo, apike, afue kisha useme eti hajachoka. huo sasa ni udhalilishaji na utumwa uliopitiliza na kutothamini kile anachokifanya mwanamke anaebaki nyumbani.

    Hebu jaribu weekend moja mwambie mkeo leo nenda katembee kwenu urudi jumatatu, halafu wewe hiyo weekend ufanye kazi zote alizokuwa anazifanya mkeo uone kama kubaki nyumbani ni kula na kulala tu au kuna mtiti wa kutosha.

    ReplyDelete
  4. Huyo mwanamke anaebaki kufanya kazi za nyumbani na hana kazi ya nje ya kumuingizia kipato hata kama kachoka kama Punda ukimuomba unyumba hawezi kukukatalia kwa sababu akikataa ukimfukuza ataenda wapi? Anafanya tu basi ili angalau umpe matumizi na apate pa kulala lakini hana jinsi.

    ReplyDelete
  5. mada nzrui sana ikichangiwa bila ugomvi nadhani muandishi yuko sahihi au hayuko sahihi wanawake wa manyumbani wana raha zao na wafanyakazi wana raha zao inategemeana ila wengi wanaofanya kazi wanadharau sana wanaume zao honestly speaking huyo asie na pakwenda nae mwanaume anamnyanyasa sana mara nyingi sasa sijui kipi chema

    ReplyDelete
  6. Mada nzuri sana hongera mtoa Mada na umeelezea kwa marefu na Mapana sana mwanamke anayefanya kazi na asiyefundwa kwao ni msalaba mzito sana kwa Mumewe. Ni heri kuoa mama wa nyumbani ambaye hata akiomba hela ya salon ni sawa kumpatia kuliko yule mke ambaye mnajihimu wote asubuh kwenda kazini na mshahara mnapata sawa kisha anakuomba hela ya salon. Nyumbani uwajibikaji ni sufuri chakula unakula cha dada wa kazi. Akirud kazin yeye na mitandao ya kijamii hana hata muda wa kumuosha mtoto akijipupulia. Sasa si ni heri mama wa nyumbani!?

    ReplyDelete

Top Post Ad