Man City Yaweka Rekodi Mpya EPL

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Klabu ya Manchester City imeweka rekodi ya kushinda mechi 10 mfululizo za ufunguzi wa ligi kuu ya Uingereza baada ya kuifunga Wolves kwa mabao 3-1,mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Molineux.

 

Mchezaji bora wa PFA msimu uliopita, Kelvin de Bruyne akishangilia baada ya kuifungia Manchester City.

 

Mabao ya Man City yalifungwa na Kelvin de Bruyne kwa mkwaju wa penati dakika ya 20, Phil Phoden dakika ya 32 na la tatu lilisukumiziwa kimiani na Gabriel Jesus dakika ya 90 .

 

Ulikua mchezo mzuri kwa kiungo Phil Phoden ambaye kwa sasa amehusika katika mabao 22 kwenye mechi 33 alizocheza, akifunga mabao 12 na pasi 10 za usaidizi wa mabao, bso pekee la wenyeji lilifungwa na Raul Jimenez dakika ya 78 ya mchezo.


Haikua mechi nzuri kwa Kocha , Nuno Espirito ambaye alikosa huduma za Matt Doherty aliyetimkia katika Klabu ya Tottenham Hotspurs, Diogo Jota alisajiliwa na Liverpool


Akizungumza baada ya mchezo Kocha wa Wolves Nuno Espirito amesema''Kipindi cha kwanza hatukuanza vizuri sana. Manchester City ilihamisha mpira vizuri na ilituletea shida nyingi. Tulikubali adhabu na kutoka hapo inakuwa ngumu zaidi. Katika nusu ya pili tuliboresha. Tuliunda wakati mwingi na nafasi ambazo tunaweza kupata kutoka. Tulijua wakati mmoja unaweza kubadilisha kila kitu.''


"Tulibadilika na kujaribu kubadilika. Tulizuia umiliki wa City na kupitia katikati. Tuliweza kushinikiza na kuokoa mpira. Tulikuwa na vitu vingi vya kubadilisha na kufanya kazi. Mbaya sana hatukumaliza na mwisho tofauti kwa mchezo ilionekana."


Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola alisema"Ilikuwa mechi mzuri. Tunajua jinsi ilivyokua mechi ngumu.Wakati mwingine ufunguzi ni mzuri na wakati mwingine tunahitaji muda zaidi kupata hali zetu bora - lakini mwanzo ulikuwa mzuri. "


Kipindi ambacho tuko nacho na hali ambayo tulikuwa nayo katika wiki hizi mbili zilizopita, nilitarajia kwamba wakati fulani tutateseka, lakini kwa jumla tulidhibiti mchezo."


REKODI MUHIMU


-Man City imekuwa timu ya kwanza kushinda michezo 10 ya ufunguzi wa Ligi Kuu mfululizo.


-Lilikuwa bao la sita kwa Raul Jimenez kwenye ligi tangu kuanza kwa msimu uliopita - hakuna mchezaji aliyefunga zaidi wakati huo.


-Man City imeshinda michezo sita ya Premier League mfululizo kwa mara ya kwanza tangu Agosti 2019 (Mechi 15).


-Mnamo mwaka wa 2020, Manchester City wamefaidika na adhabu ya mikwaju ya penati kuliko timu yoyote ya Uingereza,(nane, wakifunga nne).


-Tangu kuanza kwa msimu uliopita, De Bruyne amekuwa akihusika moja kwa moja katika ushindi wa City katika Ligi Kuu (Katika mabao 35 amefunga 14,na pasi 21 za usaidizi wa mabao) kuliko mchezaji yeyote - Matatu mbele ya Mohamed Salah wa Liverpool.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad