NASA yatangaza mpango wa kuwapeleka wanaanga mwezini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Shirika la anga za mbali la Marekani, NASA, limetangaza mpango wa kutuma tena wanaanga mwezini, kwa gharama ya takribani dola bilioni 28. Kati ya hizo, chombo cha kuwapeleka wanaanga hao kitagharimu dola bilioni 16. 

Mpango huo ulianzishwa na rais Donald Trump kama mojawapo ya vipaumbele vya utawala wake, utahitaji idhini ya bunge la nchi hiyo linalokabiliwa na uchaguzi wa mwezi Novemba. 


Gharama hiyo ya Dola bilioni 28 inapaswa kupatikana katika bajeti ya miaka minne kati ya 2021 na 2025. 


Katika mazungumzo na waandishi wa habari, mkuu wa NASA Jim Bridenstine amesema hofu za kisiasa ni changamoto kubwa kwa kazi ya shirika lake. 


Rais wa zamani Barack Obama aliufuta mradi wa kupeleka wanaanga katika sayari ya Mars, baada ya mtangulizi wake kutumia mabilioni ya dola kuuandaa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad