Picha: Aubameyang Amaliza Ukimya Kwa Vitendo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Hatimaye Nahodha na Mshambuliaji wa klabu ya Arsenal ya England, Pierre Emerick Aubameyang amesaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo yenye maskani yake makuu Kaskazini mwa jijini London.

Mshambuliaji huyo kutoka nchini Gabon amesaini mkataba mpya, baada ya kukamilisha mazungumzo na uongozi wa klabu hiyo, ambao ulionyesha kila sababu ya kutaka kuendelea kufanya kazi na nyota huyo, ambaye alisajiliwa klabuni hapo mwaka 2018, akitokea Borussia Dortmund chini ya utawala wa babu Arsene Wenger.

Aubameyang mwenye miaka 31 ataendelea kuwa sehemu ya kikosi cha Arsenal hadi mwaka 2023, baada ya kusaini dili hilo ambalo litamfanya awe analipwa mshahara wa Pauni 250,000 kwa juma.

Aubameyang amesema:”Mwisho wa siku nimesaini bonge moja ya saini, nina furaha kuwa ndani ya Arsenal.  Hapa ni nyumbani na ni furaha kwangu.

“Siku ya leo (jana) ni kubwa kwangu na ninahitaji kuwa Legend ndani ya Arsenal na nitakapoondoka niache alama. Ni muda wangu wa kazi na nitapambana.”

Kabla ya kusaini mkataba mpya jana Septemba 15, Aubameyang alihusishwa na taarifa za kuwaniwa na klabu za ndani na nje ya England, huku manguli wa Ligi ya nchini Hispania Real Madrid na FC Barcelona walikua wakitajwa mno na vyombo vya habari.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad