Pigo za Kike Zamponza Msanii Rayvanny

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Staa wa Bongo Fleva anayeitumikia Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB), Raymond Mwakyusa ‘Rayvanny’, anadaiwa kubadilika kidogokidogo kila kukicha kutoka kwenye ule mwonekano wake wa kiume na sasa anatia shaka kiasi cha kuibuliwa skendo nzito kutokana na mapigo yake ya kike.

Tangu alipodaiwa kuachana na aliyekuwa mzazi mwenzake, Fahima Msenga ‘Fahyvanny’ aliyezaa naye mtoto mmoja wa kiume aitwaye Jaydan, amekuwa hasomekisomeki huku mwonekano wake wa kike ukizua maswali mengi. Baadhi ya mashabiki wa Rayvanny au Vanny Boy, sasa wanaonesha kuwa na shaka juu ya mwonekano huo; baadhi yao wakihoji kama kweli yupo sawa?

Miezi kadhaa iliyopita, Vanny Boy alianza kutupia picha zikimuonesha akiwa amevaa mawigi ya wanawake kichwani, huku mwenyewe akitamba kuwa ni mwonekano mpya.

Mwonekano wake wa wikiendi iliyopita akiwa ametengeneza nywele kama mwanamke, uliibua gumzo kubwa kwenye mitandao ya kijamii, huku wengine wakimtolea maneno ya kashfa yasiyoandikika gazetini.


Kwa mujibu wa baadhi ya wafuasi wake wapatao zaidi ya milioni 5.5 kwenye ukurasa wake wa Instagram, mwonekano huo ulimfanya kuonekana mrembo mno na kupoteza ule ugumu wake wa kiume kama zamani.


 


Baadhi ya mashabiki wake hao, walikuwa na maoni haya;


Iamdanny_tz: “Duh mzee baba bado hujaingia system ya vipara….Naona style za nywele zote unamaliza.


Neylioutfittz: “Yaani mpaka umenizidi urembo.”


Kiiss_raj_tz: “Umekuwa kama….(jina la mwanamke).”




Sistadready: “I’ve so far loved your fashion, touch of style, both modern and classic old but I don’t really know about this hair. I kinda feel it’s too female, well, I don’t know.”


Furnituremsukuma: “Utavaa hadi nguo ya ndani mwaka huu.”


Sofia_manyinyi: “I really luv ur hair.”


Gilbertnday: “Unajua kuimba na muziki wako ni mzuri, ila style ya kuvaa aisee hapana kaka.”


Adija Niyonkuru: “Hizo styles za wanamuziki wa Kimarekani very nice. Yeye ni star.”

Akizungumzia mwonekano huo, Vanny Boy amesema kuwa, hakuna lolote zaidi ya mtindo mpya wa kiume wa nywele zake na kwamba, umekuwa ni utaratibu wake wa kuzibadilisha mara kwa mara.

Hata hivyo, baadhi ya mashabiki wamemtaka Vanny Boy kurudi kwenye fasheni yake ya zamani ya virasta, kwani ilikuwa ikimpendeza zaidi kuliko hii ambayo inamsababishia kutiliwa shaka.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad