Polepole Awaonya Wagombea na Siasa za Kusemana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole, amewaonya viongozi na wagombea wa nafasi mbalimbali katika chama hicho wajiepushe na siasa za kusema watu badala yake wajikite kufanya siasa zenye kuzingatia ustaarabu.

Amesema hayo leo Agosti 31, 2020, wakati akitaja majina ya wagombea wa uwakilishi kwa upande wa Zanzibar na kusema kuwa kwa upande wa Tanzania Bara wamezindua kampeni zao vizuri kwa kuwasilisha hoja zao kwa Watanzania.

"Tufanye siasa za kistaarabu,na sisi tumezindua kampeni juzi vizuri kabisa hatutaki kusema watu ,tunasema hoja tunaziwekea sababu na tunaeleza tunachotaka kupeleka kwa watanzania", amesema Polepole

Akimzungumizia mgombea Urais kwa upande wa Zanzibar Polepole amesema, "Tumempata mtu mmoja mpole,mtaratibu, mtu wa watu, mwenye nidhamu ya hali ya juu ambaye amehudumu kwenye dhamana ya uongozi kama kiongozi mwandamizi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano, ni Mzanzibari kwelikweli ndugu yetu Hussein Mwinyi”.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad