Poshy: Wanawake Wanaongoza Kwa Chuki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mrembo ambaye alijizolea umaarufu hivi karibuni baada umbo lake kuonekana kuwavutia watu mbalimbali bongo, Jacqueline Obeid ‘Poshy’ amesema alichojifunza kwenye dunia hii, wanaoongoza kwa chuki na roho mbaya ni wanawake na sio wanaume.


Akizungumza na Amani, Poshy, alisema kuwa amegundua kuwa kuna wanawake wengine hawapendi kuona mwingine anaendelea hivyo mwanamke huyo akiona mwenzake anapiga hatua, atamuwekea kila aina ya chokochoko ili kumtibulia mambo yake.



“Watu wanashindwa kuelewa kuwa huku duniani kila mtu ana bahati yake hivyo ukiona mwenzako anafanikiwa au mwanamke mwenzako anafanya vizuri mshike mkono uzidi kumfanya ainuke ili akuinue na wewe na sio kumponda kila kukicha maana huo utaitwa ni wivu,” alisema Poshy ambaye tayari amejikwamua kwa kufungua duka lake la kuuza nguo za ndani.

Stori: Imelda mtema
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad