AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Jeshi la Polisi limekamata raia saba wa kigeni kwa kosa la wizi wa mitandaoni. Watuhumiwa hao raia wa Nigeria, Liberia, DRC, India na Afrika Kusini wenye umri kati ya miaka 28 na 44 walikamatwa kati ya mwezi Agosti na Septemba mwaka huu.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam SACP Lazaro Mambosasa, amesema watuhumiwa hao wamekiri kujipatia kiasi cha shilingi milioni kumi (Tsh 10,000,000/=) kihalifu, na kutumia pesa hizo kufungua duka la pombe kali, kununua gari aina ya MARK II, runinga mbili na magodoro.
Aidha, Mambosasa amesema wapo katika msako wa kuwatafuta Watanzania walioshirikiana na wahalifu hao. Na kuwataka wageni wote wanaoingia nchini kwetu kufuata sheria zilizopo.
Watuhumiwa wote bado wanashikiliwa na polisi na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK