Rais wa Afrika Kusini azitaka nchi tajiri kusaidi uchumi wa nchi za Afrika

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, ambaye pia ni mweneyekiti wa Umoja wa Afrika ametoa wito kwa mataifa ya dunia kuyasaidia mataifa ya Afrika kujikwamua kiuchumi, kutokana na janga la Corona.


Kiongozi huyo wa Afrika Kusini ambaye nchi yake imeathirika zaidi kutokana na idadi kubwa ya mamabukiziii ya virusi vya Corona, ameonya kuwa iwapo mataifa ya Afrika hayatasaidiwa ikiwa ni pamoja na kufutiwa madeni, yataendelea kuyumba kiuchumi kwa kipindi kirefu.


Kauli hii inaendana na ile ya rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi, ambaye ameyataka mataifa tajiri kusamehe madeni kwa nchi masikini, ikiwa ni pamoja na Afrika wakati huu nchi nyingi zikikabiliwa na janga hatari la Corona.


Licha ya mataifa tajiri zaidi ya 20 na Shirika la Fedha Duniani, IMF, kusema kuwa yanatathmini cha kufanya kuyasaidia mataifa hayo, rais Thsisekedi katika ujumbe wake kwa viongozi wa dunia kupitia njia ya video, ametaka kufutwa kabisa kwa madeni hayo.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad