Serikali Yakanusha Watendaji Wa Halmashauri Kuitwa Dodoma Na Dkt. Magufuli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Ofisi ya Rais – TAMISEMI imekanusha taarifa iliyotolewa na Mgombea Urais kupitia CHADEMA kwa kusema kuwa Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri nchi nzima wameitwa jijini Dodoma na Mgombea Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli


Taarifa iliyotolewa imesema, Ofisi ya TAMISEMI ndiyo inayosimamia Watendaji wote Nchini na tuhuma alizozitoa Lissu ni za Uongo na Wananchi wote wanapaswa kuzipuuza kwasababu hazina ukweli wowote. Watendaji wote wapo katika vituo vyao vya kazi


Lissu alisema Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri ndio Wasimamizi wa Uchaguzi hivyo kitendo cha kuitwa na Dkt. Magufuli kimempa wasiwasi kwamba wanakwenda kupewa maelekezo ambayo yanaweza kuleta matokeo yaliyotokea katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019.


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Tamisemi, Joseph Nyamhanga akizungumzia taarifa iliyotolewa na Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema kuhusu wakurugenzi wa halmashauri zote kuitwa Dodoma.




-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad