Shilole, Mume wa Mtu Utamu Kolea!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



LICHA ya staa wa Bongo Fleva ambaye pia ni mjasiriamali, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ kutotaka kuzungumzia uhusiano wake na mume wa mtu ambaye ni mpiga picha anayefahamika kwa jina Rommy3D, wawili hao wamezidi kunogesha ukaribu wao kwa mapichapicha ya kimalovee.


 


Ukiachana na picha ya awali ambayo ilivuja ikiwaonesha wakiwa kwenye sherehe pamoja, mapema wiki hii zilivuja nyingine zilizowaonesha wakiwa kwenye ‘mkao wa mtu mtuwe’ huku Shilole akionekana kumkata jicho flani ‘ameizing’ Rommy.


 


“Mh! Mwenzangu mambo ni moto, hapa hata kama huwezi kusoma hata picha tu inajieleza kwamba, hapa kuna kitu,” alichangia mdau mmoja kwenye Instagram, huku wengine kibao wakishadadia ishu hiyo. Akizungumza na gazeti ndugu na hili la IJUMAA WIKIENDA, Shilole alipoulizwa kama ni kweli wana uhusiano na mume huyo wa mtu, alisema aachwe, aulizwe vitu vya msingi tofauti na ishu hiyo ya mahusiano.


 


Hata hivyo, watu wa karibu na Shilole, wamedai kuwa mrembo huyo kwa sasa wapo kwenye hatua nzuri ya mahusiano, hivyo siku si nyingi wataweka kila kitu hadharani.


 


Kwa upande wake mke wa Rommy3D alipozungumza na gazeti la IJUMAA WIKIENDA juzi, alikuwa mkali na hakutaka hata kujitambulisha jina lake kamili. “Jamani mimi sijaona hizo habari wala nini, na kwa nini mje mniulize mimi hayo mambo? “Kwa nini msiwaulize wahusika? Naombeni mniache, nipo mazoezini,” alisema.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad