Sumaye aishukia CHADEMA, asema hawawezi kuongoza nchi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Frederick Sumaye amesema vyama vya Upinzani nchini haviwezi kuongoza nchi kwa sababu hawana sera.


Ameyasema hayo Leo septemba 30,2020 akizungumza na wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini katika mkutano wa Mgombea Mwenza Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia  Suluhu Hassan kunadi Sera za  Chama cha Mapinduzi katika viwanja Vya Haydom.


Sumaye amesema Chama alichotoka  CHADEMA,  ni Chama cha Uwana harakati na hakina sera  zozote za kuwasaidia wananchi.


'CHADEMA wanafikiri kuwa nchi ya Tanzania bado ipo  mikononi mwa  Wakoloni, wanapiga kelele utafikiri bado tunatawaliwa' alisema Sumaye


'Nilienda kule  lakini baada ya kugundua hawana chochote nikaamua kurejea nyumbani' alisisitiza Sumaye


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Manyara Simon Lulu amesema Chama hicho kinajiandaa kwa ushindi wa kishindo kwa sababu kimefanya maendeleo kwa wananchi.


Amemweleza Mgombea Mwenza kiti  cha Urais Tanzania Samia Suluhu Hassan kwamba katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika oktoba 28 mwaka huu, Upinzani mkoani hapo hawataambulia hata kiti  cha Udiwani.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad