Tajiri Mkosoaji wa Rais Ahukumiwa Kifungo cha Miaka 18 Jela China

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Korti moja nchini China imetoa hukumu ya kifungo cha miaka 18 jela kwa tajiri mmiliki wa majengo Ren Zhiqiang, ambaye ni mkosoaji wa rais wa nchi hiyo, Xi Jinping. 

Korti hiyo ya mjini Beijing imemkuta tajiri huyo na hatia ya rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma. Ren mwenye umri wa miaka 69 alikuwa mwanachama wa chama tawala cha kikomunisti, na mwenyekiti wa kampuni ya Huayuan Properties, na alikuwa na urafiki na maafisa waandamizi wa chama hicho, akiwemo makamu wa rais Wang Qishan. 


Mapema mwaka huu, tajiri huyo na mwanawe walitoweka kwa muda, baada ya kutunga shairi lililokosoa namna serikali ya rais Xi Jinping ilivyolishughulikia janga la virusi vya corona. 


Alifukuzwa kutoka chama tawala mwezi Julai, akituhumiwa kula njama na watoto wake za kujirundikia mali bila kikomo. Korti hiyo imesema Ren Zhiqiang amekiri makosa yake na kuomba msamaha.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad