Tetesi za Usajili wa Samatta Ulaya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Klabu ya West Brom Albion ya nchini Uingereza inajaribu kuna saini ya mshambuliaji wa Aston Villa, Mbwana Samatta ambaye ameripotiwa kuwa anaelekea nchini Uturuki.

Klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya England inataka kumnasa nahodha huyo wa Tanzania mwenye umri wa miaka 27 ambaye anafanya mazungumzo ya kuhamia Fenerbahce.

Taarifa kutoka Uingereza zinazeleza kuwa West Brom watamchukua Samatta ama kwa mkopo au kumnunua endapo dili litafanikiwa kwani tayari Villa wameonesha kumruhusu kuondoka.

Fenerbahce imekuwa ikimmendea nyota huyo lakini Albion wanaamini kuwa wanaweza kukatisha safari yake ya Uturuki na kumbakisha Uingereza.

Samatta alijiunga Villa Park akitokea Genk ya Ubelgiji Januari mwaka huu baada ya Wesley kupata majeraha. Mkataba wake na Villa unamalizika 2024.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad