Uingereza yapandisha ngazi ya kitisho cha COVID-19

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Uingereza imepandisha kiwango cha tahadhari juu ya kitisho cha maambukizi wa virusi vya corona kutoka ngazi ya tatu hadi ya nne, kutokana na kuongezeka kwa kasi ya maambukizi mapya. 

Ngazi ya nne maana yake ni kwamba hatari ya kuambukizwa virusi hivyo ni ya kiwango cha juu. Wataalamu wa afya nchini humo wameonya kuwa ikiwa hatua madhubuti hazitachukuliwa, Uingereza itaanza kushuhudia ongezeko la vifo kutokana na ugonjwa wa COVID-19. 


Mganga mkuu wa serikali ya England Chris Whitty amesema ifikapo katikati mwa mwezi ujao wa Oktoba, huenda Uingereza itakuwa ikisajili maambukizi mapya 50,000 kila siku. 


Tayari Uingereza ndio nchi iliyoathiriwa zaidi na COVID-19 barani Ulaya, ikiwa imewapoteza watu wake 42,000 kwa janga hilo. 


Waziri mkuu wa nchi hiyo Boris Johnson ametangaza mkakati mpya wa kuzuia kasi ya kuenea zaidi kwa ugonjwa huo, zikiwemo kupunguza muda wa huduma za baa na mikahawa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad