Africa ‘haiwezi kuhimili’ wimbi la pili la virusi vya corona

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Shirika la afya duniani (WHO) limeonya kuwa Afrika haiwezikuhimili wimbi la pili laCovid-19, likisema kuwa litakuwa na athari kubwa hususan za kiuchumi.


Onyo hilo linatolewa wakati maambukizi yakiendelea kuongezeka katika nchi nyingi ambazo zililegeza sheria za kupambana na maambukizi hayo hivi karibuni.


WHO linasema virusihavitaweza kudhibitiwakama mataifa ya Afrika yataendelea kufungua shughuli zakebila kuweka tahadhari za kuzuwia maambukizi ya virusi vya Corona.


Imeonya pia juu ya kurejea kwa vipindi vya amri za kutotoka nje ambazo inasema Afrika haiwezi kuvihimili.


Mkurugenzi wa Who kanda ya Afrika, Matshidiso Moeti, pia amesema hatua zimewekwa kuhakikisha bara hilo linapata sehemu yake ya ya chanjo yoyote inayotengenezwa.


Afrika imeripoti zaidi yavisa milioni 1.6 vya virusi vya corona tangu mlipoko huo ulipoanza huku watu 39,000 wakifa kutokana na maradhi hayo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad