Al Ahly Watinga Fainali Mabingwa Afrika

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



KIGOGO wa soka kutoka Morocco, Wydad Casablanca, amekubali kapigika nje-ndani kwenye mtanange wa nusu fainali ya ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya bingwa wa kihistoria wa michuano hiyo National Al Ahly ya Misri.


 


Akiwa nyumbani Wydad alitunguliwa 2-0, juma lililopita na usiku wa jana Ahly akaonyesha umwamba akiwa kwenye uwanja wa nyumbani  baada ya kushinda magoli 3-1.


 


Al Ahly wametinga fainali kwa jumla ya ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Wydad na sasa anamsubiri mshindi baina ya Zamalek ambaye anaoongoza mechi ya mkondo wa kwanza kwa ushindi wa  1-0 dhidi ya Raja.  Mtanange huo utachezwa Novemba Mosi, wakati fainali itachezwa Novemba 6 mwaka huu.


 


Haya ni mafanikio ya kocha mpya kutoka Afrika ya Kusini, Pitso Mosimane, ambaye amejiunga na Klabu hiyo hivi karibuni akitokea Mamelodi Sundowns.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad