AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mahakama ya juu huko Lilongwe, nchini Malawi imemuhukumu Uladi Mussa, aliyekuwa waziri mwenye ushawishi mkubwa nchini humo kifungo cha miaka mitano gerezani kwa kutumia vibaya madaraka yake.
Mussa alikamatwa kwa kosa la kuwasaidia raia wa kigeni kupata uraia na pasipoti za Malawi kwa njia za ulaghai alipokuwa waziri wa mambo ya ndani chini ya utawala wa aliyekuwa rais Joyce Banda.
Watatu waliokuwa maafisa wa uhamiaji ambao pia walihukumiwa na Mussa, nao wamehukumiwa kifungo cha kati ya miaka mitatu na sita.
Mussa alikuwa mbunge ambaye amehudumu katika nyadhifa mbalimbali za mawaziri chini ya utawala wa marais wanne tofauti.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK