AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Chama cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Babati Mjini kimepita kwa kishindo katika nafasi ya Udiwani kwenye kata zote nane za Jimbo hilo lililopo mkoani Manyara.
Kabla ya Uchaguzi mkuu kufanyika Kata za Nangara na Babati Mji zilikuwa zinashikiliwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Akitangaza matokeo hayo Msimamizi wa Uchaguzi Jimboni hapo Fortunatus Fwema amesema Madiwani hao wanasubiri kupatiwa Vyeti vya kutambuliwa na baadaye kuapishwa rasmi.
Pamoja na hayo, Msimamizi huyo amemkabidhi cheti cha utambuzi Mbunge Paulina Gekul (CCM) aliepita bila kupingwa.
Jimbo la Babati Mjini lina kata nane ambao ni Maisaka, Mutuka, Sigino,Bonga,Nangara, Singe, Bagara na Babati Mji.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK