Kamanda Muroto “Polisi tumewezeshwa kufanya doria”

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, SACP Gilles Muroto amesema kuwa kuelekea uchaguzi mkuu usalama wa raia na mali zao umeimarishwa katika mkoa huo.


Muroto amesema hayo muda mfupi uliopita jijini Dodoma na kusema kuwa katika kufanikisha jambo hilo Jeshi la Polisi mkoani humo litashirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kama Jeshi la Magereza,Mgambo ,Uhamiaji na Zimamoto.


“Tayari Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Binilith Mahenge ametuwezesha usafiri kwa ajili ya kufanya doria na kusafirisha vifaa mbalimbali vitakavyotumika kwenye uchaguzi huo kutoka sehemu moja kwenda nyingine ” Kamanda Muroto.


Aidha, Kamanda Muroto amesema kuwa kutakuwa na askari kwa kila kituo kidogo cha kupigia kura ambao wote kwa pamoja watakutana sehemu kuu ya majumuisho ili kuhakikisha usalama wa sehemu husika unaimarika.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad