Kiongozi wa Upinzani Guinea Ajitangaza Mshindi Kabla ya Matokeo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Kiongozi wa upinzani nchini Guinea, Cellou Dalein Diallo, amejitangaza mshindi katika uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili kabla ya kutangazwa kwa matokeo rasmi.

Bwana Diallo aliwaambia wanahabari na wafuasi wake kwamba ameshinda duru ya kwanza ya uchaguzi.


Hakutoa takwimu zozote lakini amesema kuwa hitimisho lake ni kutokana na hesabu ya chama chake wala sio tume rasmi ya uchaguzi.


Tume ya uchaguzi imejibu kwa kusema shughuli ya kuhesabu kura bado inaendelea na hiyo ndio pekee yenye mamlaka ya kumtangaza mshindi.


Wafuasi wa Bwana Diallo ambao walikuwa wamekusanyika kusherehekea walitawanywa na maafisa wa polisi. Baadae aliandika ujumbe kwenye Twitter kwamba watu watatu wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa na polisi.


Raia wa Guinea wamekuwa wakiandamana kwa miezi kadhaa sasa tangu Rais Alpha Condé alipotangaza kuwania muhula wa tatu.


Matokeo ya uchaguzi huo uliotanda wasiwasi yanatarajiwa kutolewa Jumatano na baada ya hapo wagombea watakuwa na siku nane za kukata rufaa ikiwa wana malalamiko yoyote.


Mgombea wa urais anahitaji zaidi ya asilimia 50 ya kura kupata ushindi wa moja kwa moja au kutakuwa na duru ya pili ya uchaguzi Novemba 24.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad