Mama wajawazito wajifungulia njiani, kulikoni ?

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Wananchi wa mtaa wa Mangaya uliopo Mbagala, Jijini Dar es Salaam, wameiomba serikali kuitengeneza barabara ya Shimo la mchanga ambayo imeharibika vibaya na kushindwa kupitika kwa urahisi hali ambayo inasababisha wakati mwingine hata wajawazito kujifungulia njiani.



Wakiongea na Kurasa leo wananchi hao wamesema kinamama wajawazito wamekuwa wakijifungulia njiani kutokana na ubovu wa barabara hiyo huku wakieleza kwamba mvua inaponyesha ndio inashindwa kupitika kabisa hali inayosababisha hata magari yanapopita kuharibika.


“Hali ya barabara hii ni mbaya sana tunapata shida sana sisi wakazi wa huku hivyo serikali ituangalie kwa jicho la huruma” amesema Zalia Habibu mkazi wa Mangaya


Amesema tayari kilio chao hicho wamekifikisha kwenye ngazi ya serikali ya mtaa na waneahidiwa kutengenezwa kwa barabara hiyo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad