google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Mapokezi Ya Zitto Kigoma Siku Kadhaa Baada Ya Ajali | UDAKU SPECIAL

Mapokezi Ya Zitto Kigoma Siku Kadhaa Baada Ya Ajali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mgombea ubunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe leo Ijumaa Oktoba 16, 2020 amewasili  mkoani Kigoma ikiwa zimepita siku 10 tangu alipopata ajali ya gari mkoani humo na kuhamishiwa Dar es Salaam kwa matibabu.


Zitto ambaye ni kiongozi wa chama hicho alipata ajali Oktoba 6, 2020 mkoani humo wakati akielekea katika mkutano wa kampeni jimbo la Kigoma Kusini, akiwa na watu wengine wanne.


Baada ya kufika jijini Dar es Salaam, Zitto alipelekwa katika Hospitali ya Aga Khan na kufanyiwa upasuaji katika bega lake la kushoto.


Leo katika uwanja wa ndege mjini Kigoma wanachama na wafuasi wa chama hicho walifika eneo hilo kuanzia saa 3 asubuhi kwa lengo la kumlaki kiongozi wao huyo ambaye baada ya kushuka kwenye ndege alipokelewa na wanachama hao huku akiwashukuru kwa kumuombea.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad