Mboto Agoma Carlinhos Kuitwa Mkata Umeme

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



ALIYEKUWA mjumbe wa kamati ya hamasa ya Yanga, Mboto Haji, amesema Carlos Fernandes de Carmo ‘Carlinhos’ ndani ya kikosi cha timu hiyo ni mng’oa nguzo na siyo mkata umeme.


Mchekeshaji huyo aliyazungumza hayo baada ya mchezo wa kirafi ki dhidi ya Mwadui FC, uliopigwa kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi jijini Dar ambapo Yanga ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0.


Katika mtange huo, mshambuliaji wa klabu hiyo, Michael Sarpong, ndiye aliyeibuka kuwa mchezaji bora ambapo alipachika bao pekee la ushindi dakika ya 81 ya mchezo baada ya kupokea pasi kutoka kwa Carlos Carlinhos.


Akizungumza na Championi Jumatatu, Mboto alisema kuwa kwa sasa timu hiyo ina wachezaji wazuri kutokana na usajili uliofanyika jambo ambalo linapelekea wachezaji kucheza ‘pira biriani’.


“Yanga tuna wachezaji wazuri baada ya kufanya usajili ambao una tija kutokana na aina ya wachezaji waliopo ukimwangalia Carlinhos akiingia uwanjani ni mng’oa nguzo na siyo mkata umeme kama wanavyomuita,” alisema Mboto.


LEEN ESSAU, Dar es Salaam

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad