Ndugu wa Bilionea Laizer Waanika Mlinzi Alivyouawa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


NDUGU na Meneja wa Bilionea Laizer aitwaye Kiria Laizer amethibitisha taarifa za kifo cha mlinzi wa mgodi wa bilionea huyo kilichotokea usiku wa saa 9 kuamkia siku ya Jumatatu ya Septemba 28, 2020, huko mgodini mahali ambapo alikuwa anafanyia kazi.

 

Kiria Laizer amesema tukio hilo limefanyika ndani ya ukuta wa Mererani ambapo mlinzi huyo alipigwa na kitu chenye ncha kali kichwani  na kwa sasa kesi hiyo ipo mikononi mwa polisi.

 

“Tulienda kwenye eneo la tukio tukamkuta marehemu pembeni mwa hema la kuhifadhia zana, tukamkuta amelala nje na alikuwa tayari ameshapoteza maisha ambapo alikuwa na jeraha kubwa kwenye kichwa;  kwa harakaharaka unaweza kusema amepigwa na kitu chenye ncha kali,” ameeleza Kiria Laizer.

 

“Mwili bado haujazikwa kwa sababu familia ina utaratibu wao ambao wanaendelea nao na wakiwa tayari taratibu za mazishi zitafanyika, kwa sasa hatuna ripoti yoyote ya polisi bali uchunguzi bado unaendelea,” ameongeza.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad