google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Raia wa kigeni wakamatwa wakiingiza dawa za kulevya Ethiopia | UDAKU SPECIAL

Raia wa kigeni wakamatwa wakiingiza dawa za kulevya Ethiopia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Polisi nchini Ethiopia wamewakamata washukiwa 14 kwa kujaribu kuingiza dawa za kulenya aina ya kokeini kupitia uwanja mkubwa wa ndege mjini Addis Ababa.

Polisi nchini humo wamesema washukiwa 13 raia wa Nigeria na mmoja wa Brazil wamepatikana na kilo 14 za dawa za kulevya aina ya kokeini katika mabegi yao, nguo za ndani na baadhi zilikuwa wamezimeza.


Washukiwa hao walikuwa wamewasili Sao Paulo, Brazil, Jumatatu.


Walikamatwa na kuzuiliwa uwanja wa ndege, kwa mujibu wa kamanda anayeshughulikia oparesheni ya dawa za kulevya Mengisteab Beyene.


Polisi waliongeza kusema kuwa Ethiopia imenasa kilo 39 za dawa za kulevya aina ya kokeini na kilo 36 za bangi kwa kipindi cha miezi mitatu iliyopita

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad