Rusesabagina Anyimwa Dhamana Mahakama Rwanda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mahakama ya juu mjini Kigali jana imekataa ombi la dhamana la Paul Rusesabagina, ikiagiza abaki kizuizini ili ashtakiwe kwa kuhusika na vitendo kadhaa ikiwa ni pamoja na ugaidi. 

Rusesabagina amekuwa akiishi uhamishoni kwa miaka mingi na alikua mkosoaji mkubwa wa serikali Rwanda. 


Lakini mnamo Agosti ghafla alijikuta amefikishwa mjini Kigali baada ya kukamatwa katika mazingira ya kutatanisha, na familia yake inadai alitekwa nyara na kupelekwa Rwanda. 


Lazima ajibu mashtaka 13 ikiwa ni pamoja na ugaidi, ufadhili na kuanzisha vikundi vya wanamgambo, mauaji, uchomaji moto na njama ya kuhusisha watoto katika vikundi vyenye silaha wakati wa mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994. 


Uamuzi huo umetolewa na mahakama baada ya Rusesabagina mwenye umri wa miaka 66 kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa awali wa kunyimwa dhamana, akitaja sababu za kiafya.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad