google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Simba yaiadhibu JKT Tanzania | UDAKU SPECIAL

Simba yaiadhibu JKT Tanzania

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya soka Tanzania bara, Klabu ya Simba imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya JKT Tanzania FC katika mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.

Mshambuliaji Medie Kagere aliipatia Simba bao la kwanza kwa kichwa dakika ya tatu baada ya kumalizia mpira uliopigwa na kiungo Rally Bwalya.

Dakika tatu baadaye Chris Mugalu aliifungia Simba bao la pili kwa kichwa, baada ya kumalizia krosi iliyopigwa na Luis Miquissone

Kagere tena akatupia bao la tatu dakika ya 40 kwa shuti kali la mguu wa kushoto akipokea pasi mpenyezo iliyopigwa na Clatous Chama

Dakika ya 54 Luis Miquissone alitupia bao la nne kwa shuti kali la mguu wa kushoto nje ya 18 kufuatia shuti la Kagere kuzuiwa na walinzi wa JKT Tanzania.

Mwamuzi Hance Mabena kutoka Tanga aliwaonya wachezaji Miquissone na Pascal Wawa kwa kuwaonyesha kadi ya njano kutokana mchezo usio wa kiungwana.

Ushindi huo unaifanya Simba kufikisha alama 13 sawa na watani wao Yanga wakiizidi alama moja Azam FC ambayo usiku inacheza na Kagera Sugar

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad