Taharuki! Mafuvu ya Watu 6 wa Familia Moja Yakutwa Mlimani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



MABAKI ya mafuvu na miili ya watu sita wa familia moja wakazi wa Kijiji cha Kakese Mbugani wilaya ya Mpanda mkoan Katavi, waliopotea katika mazingira ya kutatanisha miezi miwili iliyopita, imeokotwa maeneo ya milimani ambako wananchi huwa wanafanya shughuli ya kuchimba mawe na kokoto.


 


Familia hiyo ilipotea miezi miwili iliyopita huku ndugu jamaa na marafiki kwa kushirikiana na mamlaka husika, walifanya jitihada za kuwatafuta bila mafanikio jambo ambalo lilileta hofu kubwa kwa wakazi wa kijiji hicho.


 


Wananchi waliendelea kufanya uchunguzi na kuikuta miili hiyo mlimani na waliweza kuzitambua nguo za marehemu ambazo walikuwa wakizivaa wakati wa uhai wao.


 


Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi Benjamini Kuzaga, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema jeshi hilo linaendelea na uchunguzi ili kuwabaini watu waliohusika na mauaji hayo ya kikatili.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad