Tundu Lissu aendelea na kampeni zake Singida

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



 Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo,( CHADEMA) Tundu Lissu,amewataka wananchi kuchagua serikali itakayosimamia haki,uhuru na maendeleo ya watu.

Akizungumza hii leo Oktoba 11,2020,katika Kampeni zake zilizofanyika katika eneo la Iguguno Iramba Mashariki, Mkoani Singida, mgombea huyo amewataka wananchi hao kuacha kulalamika badala yake wachukue hatua ili waweze kupata maendeleo yenye maana kwao.

 ‘’Kama unataka kuwa huru  kuuza biashara  zako ukiwa huru,uuze chochote unachozalisha ukiwa huru chagua Tundu lissu’’amesema Tundu Lissu,

‘’Mtoto wako akienda shuleni au hospitali atendewe haki na sio kununua haki, mama lishe atendewe haki na bodaboda atendewe haki’’ameongeza Tundu Lissu

Aidha Lissu amesema kuwa hata kwenye maandiko Matakatifu yameandika  haki huinua taifa hivyo taifa  litainuka kukiwa na haki na tukiwa huru.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad