Ukipoteza Pasi Yanga Faini, Kaze Apiga ‘Stop’ Chips

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



INAELEZWA kuwa, Kocha Mkuu wa Yanga, Cedric Kaze, amewaam-bia wachezaji wa kikosi hicho kuwa makini wawapo mazoezini na kwenye mechi kwani akitokea mtu amepoteza pasi kizembe, basi huenda akapigwa faini.

Kaze raia wa Burundi, ameanza kuinoa Yanga Jumamosi iliyopita akichukua mikoba ya Zlatko Krmpotic raia wa Serbia ambaye ametimuliwa Oktoba 3, mwaka huu.

Taarifa kutoka ndani ya Yanga zinasema kuwa, Kaze ambaye ni muumini mkubwa wa soka la kasi na pasi nyingi, amewaambia wachezaji wake kuwa makini wawapo uwanjani kwa lengo la kumiliki sana mpira na kutowapa nafasi wapinzani kutawala mchezo.

“Kocha anataka kuona falsafa zake zinafanikiwa, hivyo basi amewaambia wachezaji kuwa makini katika kumiliki mpira na wasipoteze kirahisi.

“Atakayebainika kupoteza mipira kirahisi basi atapigwa faini ingawa mwenyewe hajaweka wazi hiyo faini ni kiasi gani,” alisema mtoa taarifa huyo.

Katika hatua nyingine, uongozi wa Yanga hadi jana jioni ulikuwa ukihangaika kusaka vibali vya kazi kwa ajili ya kocha wao huyo raia wa Burundi ili leo Alhamisi akae benchi katika mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Polisi Tanzania.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad