AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Meneja Kituo kikuu cha Mabasi Ubungo, Maira Mkama, amewatoa hofu wafanyabiashara wa kituo hicho katika suala la kuhamia katika stendi mpya ya mbezi na kusema taratibu zikikamilika basi watakuwa kipaumbele kupata nafasi ya biashara kwenye kituo hicho.
Akizungumza na kurasa hii leo Meneja huyo amesema tayari serikali imetangaza kutafuta mzabuni na kwamba baada ya kupatikana taratibu zingine zitafuata kwa wafanyabiashara watakaokidhi vigezo vilivyowekwa ili wapewe maeneo ya kufanyabiashara zao kwenye kituo hicho.
Meneja huyo ameongeza kuwa kila mwananchi ana haki ya kufanya biashara katika eneo hilo ambapo amewatoa hofu wafanyabiashara hao na kudai kuwa hakuna mgogoro wowote utakaotokea kutokana na utaratibu mzuri uliowekwa ili kugawa maeneo ya kufanyiabiashara katika eneo hilo
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK