Wapiga kura zaidi ya milioni 80 wamemaliza kupiga kura Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Zaidi ya wamarekani millioni 80 wamepiga kura ya mapema kabla ya uchaguzi wa rais wa tarehe 3 Novemba, kulingana na takwim zilizokusanywa jana na taasisi ya chuo kikuu cha Florida inayofwatilia uchaguzi wa marekani. Kiwango hicho kimevunja rekodi, ni zaidi ya asilimia 58 ya watu waliojitokeza kupiga kura kwenye uchaguzi wa mwaka 2016, na inaonyesha umuhimu wa uchaguzi wa mwaka huu ambapo kinyanganyiro ni kati ya rais Donald Trump, mrepublican na mdemocrat makamo rais wa zamani Joe Biden. Idadi kubwa ya watu walipiga kura kwa njia ya posta au kwenye vituo vya kura, kutokana na hofu kwamba virusi vya corona vinaweza kusambaa siku ya uchaguzi. Wataalamu wanatabiri kuwa idadi ya wapiga kura mwaka huu itazidi millioni 138 waliopiga kura kwenye uchaguzi wa rais wa 2016, alioshinda Donald Trump. Kura millioni 47 pekee ndizo zilipigwa kabla ya siku ya uchaguzi mwaka 2016. Imetayarishwa na Patrick Nduwimana, VOA, Washington DC


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad