Watano Familia Moja Wafariki Nyumba Ikiwaka Moto

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



WATU watano wa familia moja akiwemo mama, watoto wake watatu na wifi yake, wamepoteza maisha baada ya nyumba yao kuwaka moto majira ya saa nne usiku wa kuamkia leo katika eneo la Pugu CCM Kirumba jijini Dar es Salaam.

Baba wa familia hiyo Edward Katemi amesema moto huo ulianza majira ya saa nne usiku na waliofariki katika familia hiyo ni mke wake, Jackline Frank, mdogo wake Ester Katemi na watoto wake Edwin Katemi, Edson Katemi pamoja na Evon Katemi

Edward amesema kwa kushirikiana na majirani zake walipambana kuiokoa familia yake bila mafanikio kutokana na ukosefu wa vifaa vya kuwezesha uokoaji katika tukio hilo na waliwasiliana na watu wa kikosi cha uokoaji lakini walichelewa kufika kutokana na changamoto ya usafiri iliyokuwepo.

Kamanda wa Polisi Ilala amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema watu hao walifanikiwa kuokolewa na kukimbizwa hospitali lakini kwa bahati mbaya walipoteza maisha,  Chanzo cha moto bado hakijafahamika japo moto huo ulianzia sebuleni.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad