Afariki Dunia Baada ya Kugongwa na Treni, Kamanda Simiyu Afunguka

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Galula Luhende (50), mkazi wa Malampaka, wilaya ya Maswa, mkoa wa Simiyu, amefariki dunia baada ya kugongwa na Treni usiku wa kuamkia leo Novemba 20, 2020.

Akizungumza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, ACP Richard Abwao, amesema kuwa treni hiyo ilikuwa ikitokea Jijini Mwanza kwenda DSM na kwamba kabla ya ajali ilisimama Malampaka kupakia abiria.


“Marehemu alikuwa akidandia Treni hiyo iliyokuwa imeanza kuondoka, ndipo alipoteleza na kuanguka na kukanyagwa miguu” ACP Abwao.


“Marehemu huyo kabla ya kufariki, alikimbizwa Kituo cha Afya Malampaka na baadaye kuhamishiwa Hospitali ya wilaya ya Maswa kwa matibabu” ACP Abwao

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad