Alichokisema Mzee Msekwa kuhusu Spika Ndugai

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

  


Spika Mstaafu wa Bunge, Pius Msekwa, amesema kuwa hakuna ugumu wowote anaoweza kukutana nao Spika wa Bunge la 12, Job Ndugai, mara baada ya wabunge 19 wa CHADEMA, kufukuzwa uanachama kwa kuwa yeye ni kama daktari tu anayepokea wagonjwa kuwatibu kisha kuondoka.

 

Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na EATV&EA Radio Digital, kufuatia sakata la wabunge 19 wa viti maalum ambao wamefukuzwa uanachama na chama chao cha CHADEMA baada ya kwenda kula kiapo cha ubunge bila ridhaa ya chama, ambapo alisisitiza kuwa kwa kuwa hawana chama kilichowapeleka Bungeni basi hata ubunge wao umekoma.


"Spika Ndugai hapati ugumu wowote, hakupata ugumu walipoletwa hapati ugumu wowte wanapoondolewa yeye ni mpokeaji tu, hana ugumu na wala hafaidiki na lolote ni kama mganga wa hospitali yeye anapokea wagonjwa akiwatibu wanaondoka, wakifa wanaondoka yeye hana jukumu zaidi ya hilo", amesema Spika Mstaafu, Pius Msekwa.


Tazama video hapa chini

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hayo ni Maoni yake Msekwa. yuko huru kusema lolote.

    Hili suala, lina mizengwe na kisasi na mfumo dume na Udhalilishaji. ikiwa tunaweza kurekebisha kipengere baada ya kuona mapungufu ni bora kufanya hivyo. na hawa Waheshimiwa Wabunge wataendelea na Ubunge kama kiapo chao kilivyo.

    Chama chao kiliwateua na ni wabunge halali na kesi iko
    mahakamani. We need to protect our innocent Ladies MP's
    being Victimised..kamwe hatuto mruhusu Faru Joni na Wahuni wa Genge lake kuwapelekesha kina mama Majasiri , chama si taasisi wa Bilikana na Vibeko mateka na vibaraka Alishababu wakazi. MAONI YAACHE KWA MTOAJI.

    Waheshiwa Wabunge kuweni na Amani mko Vizuri.

    ReplyDelete
  2. Ama kweli..!! Shukurani ya Faru / (Punda) Ni MATEKE.

    Wewe mwenye Saccoz iliyo imarishwa na kujengwa na hawa Kina Mama Majasiri waliojitolea Wakati na Maisha yao kwa Ajili yenu NUSU AL FADHLA.

    Leo uone fahari na majigambo kuwatweza mbele ya umma.. kisa
    ULAJI WENU...!!!!

    Wewe na genge ako, Tuko mbioni kukuvua Uenyekiti.

    Waheshimiwa Wabunge Utawaona hivi , Mcho kumchuzi.
    tungekushauri ujiuzulu mwenyewe na Gengu lako la uchapaji RUZUKU NA MICHANGO BILA RISITI...KABLA YA PCCB & TRA h

    ReplyDelete
    Replies
    1. Muoneeni huluma , Hajitambui kwa ajili ya Sashisha
      kilikuwa kipigo kitakatifu.

      Kuna Tetesi anataka kutangaza kujiuzulu siasa ajili ya Afya na Umuri wake. Baada ya Ngome zote kufumuliwa na
      kugaragazwa.

      Na mbwana Matusi amesha Rudi kwaoooo..baada ya KUTUKANA BIG TIME..!!! YUKO NA SHOGA YAKE SIBITALI.!!

      VIOJA MTAANI..YETU MCHO NA KOMEO MKONONI UFIPA KODI.??

      Delete

Top Post Ad