Biden Apata Mafanikio yatakayomwezesha Kushinda Kiti cha Rais wa Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mgombea wa kiti cha urais kupitia chama cha Democratic nchini Marekani, Joe Biden amepiga hatua muhimu kuelekea kupata ushindi baada ya kunyakua majimbo tete ya Michigan na Wisconsin usiku wa kuamkia leo.

 Katika taarifa fupi aliyoitoa akiwa pamoja na mgombea mwenza Harris Kamala, Biden amesema hawezi kujitangazia ushindi lakini ana matumaini kuwa zoezi la kuhesabu kura litakapomalizika wataibuka kuwa washindi. 


Kwa kunyakua majimbo hayo mawili, Biden amefikisha kura 264 za Baraza maalumu la wajumbe wanaomchagua rais dhidi ya 214 za rais Doanld Trump anayewania muhula wa pili.


 Trump amezungumzia mafanikio hayo ya Biden kwa hasira na tayari amewasilisha ombi la kufungua shauri dhidi ya matokeo hayo ikiwa ni pamoja na kutaka kura kuhesabiwa tena na katika baadhi ya majimbo ametaka zoezi la kuhesabu kura kusitishwa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad