Bobi Wine Kuanza Kampeni za Urais Uganda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Kampeni za kuelekea uchaguzi kumpata rais ajaye zimeanza nchini Uganda.


Two Presidential Candidates Detained as They File to Run in Uganda - The  New York Times


Wagombea 11 akiwemo rais aliyekaa madarakani kwa muda mrefu, Yoweri Museveni ambaye atawania tena nafasi hiyo katika uchaguzi utakaofanyika katika kipindi cha miezi miwili.


Masharti makali ya kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona vimewekwa kwenye kampeni, lakini utekelezaji wake umekuwa mgumu.


Rais Museveni ameanza kampeni katika eneo liitwalo Luweero triangle, eneo ambalo lilikuwa kitovu cha vita vya msituni vya miaka mitano vilivyomuweka madarakani mwaka 1986.


Mwanamuziki ambaye sasa ni mwanasiasa Robert Kyagulanyi, maarufu Bobi Wine yuko njiano kuelekea mji wa West Nile, kuanza kampeni siku ya Jumanne.


Polisi mji wa Mashariki wa Jinja umewatawanya wafuasi wa chama cha Forum for Democratic Change(FDC) cha mgombea Patrick Amuriat Oboi kwa kutumia vitoa machozi. Walikusanyika njiani kumshangilia akielekea eneo la Mashariki kuanza kampeni yake.


Masharti ya afya wakati huu wa kampeni yanawataka wanasiasa kuepuka mikusanyiko mikubwa kwa kuwa na mkutano wa watu wasiozidi 70.


Lakini suala hili limeonekana kuwa gumu kama ilivyoshuhudiwa wakati wa uteuzi juma lililopita, wakati wafuasi wa karibu wagombea wote walipokusanyika kwa wingi kwenye mitaa mbalimbali na kwenye vituo vya biashara.


Kinyang’anyiro cha urais pia kinawahusisha majenerali wawili wa jeshi na mhitimu wa Chuo kikuu mwenye miaka 24 ambaye hana ajira.


Raia wa Uganda watapiga kura kuchagua rais na wawakilishi tarehe 14 mwezi Januari.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad