Halima Mdee na Wenzake Waitwa Kujieleza CHADEMA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA





Katibu mkuu wa Chadema, John Mnyika amesisitiza kuwa chama hicho hakikufanya uteuzi wa wanachama wao 19 ambao jana Jumanne Novemba 24, 2020 waliapishwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai kuwa wabunge wa viti maalum.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Novemba 25, 2020, Mnyika amesema chama hicho hakijateua wabunge hao wala kupeleka orodha ya majina Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), huku akitoa wito wa kuwataka wabunge hao kufika katika ofisi za chama hicho  keshokutwa Ijumaa, Novemba 27, ili kuhojiwa na Kamati Kuu ya Chama kutokana na kitendo walichokifanya.

“Tumewaita kuwaeleza kwamba Chadema hakijateua wabunge wa viti maalum wala hakijawasilisha orodha yoyote Tume Uchaguzi ya uteuzi wa wabunge wa viti maalum. Kwa katiba ya Chadema mamlaka ya uteuzi wa wabunge yako kwa kamati kuu ya chama, na kamati kuu ya chama haijawahi kufanya kikao cha uteuzi wa majina ya wabunge wa viti maalum na mimi Katibu Mkuu sijawahi kuwasilisha orodha yoyote Tume ya Uchaguzi.

“Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilituandikia barua Novemba 10, 2020 kutueleza haijapokea majina ya wabunge wa viti maalum na kutuomba kuyawasilisha ikiwemo fomu namba 8D inayopaswa kuwa na idhini ya katibu mkuu wa chama na mimi sijajaza yoyote. Niliiandika baada ya Mkurugenzi wa NEC kunukuliwa na vyombo vya habari kwamba Chadema imewasilisha orodha ya wabunge wa viti maalum na yeye amekwishaipeleka bungeni.

“Mimi kama Katibu Mkuu hakuna fomu yoyote niliyowahi kuijaza popote kuthibitisha uteuzi wa yeyote, hii fomu pia ina sehemu ya kiapo cha hakimu, kwa tafsiri nyepesi kilichofanyika ni  kughushi na wameenda kuapishwa bila baraka ya chama.

“Tumeitisha kikao cha kamati kuu Ijumaa, Novemba 27, 2020, Dar es Salaam, na tutawaandikia wahusika ili kisitokee kisingizio hakupata taarifa, natangaza wito kwa wanachama wetu 19 walioshiriki kuapishwa kufika makao makuu Kinondoni Ijumaa saa 2:00 asubuhi,” alisema Mnyika.

Aidha, amesema Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ataongoza kikao cha kuwahoji wanachama walioapishwa kuwa wabunge wa viti maalum akiongeza kwamba si mara ya kwanza wao kufanya vikao vya kinidhamu na walioapishwa wameshiriki kukihujumu chama. 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hii siyo njia sahihi ya kuwaita waandamizi.

    Si kikatiba. Hakuna wa kuja.

    ReplyDelete
  2. Barua ile tunayo, na ni wawakilishi halali katika nafasi zao halali kuwawakilisha nakuwatumikia Watanzania
    katika kipindi cha miaka 5.

    Kina Mama Wajasiri, wanyenyekevu,wachapa kazi, wajenga hoja, washiriki wa utatuzi.

    Halima/Salome/Ester/Ester..Na wateule wote.'

    Wasikubabaisheni hawa Wababaishaji.
    Tumikieni kiapo chenu cha kuwatumikia
    Wananchi kwa Miaka 5 hii 2020-2025.

    Hatuna shaka na uchapa kazi wenu.

    Wenye Wivu.... Wakashangae Ferry...!

    Halima Oyeee!!!
    Matiko / Bulaya Oyeee!!!
    Kina MAMA MNAWEZA. CHAPENI KAZI.

    HAKUNA PA KWENDA WALA PA KUJIELEZA.

    CHA MWISHO TUNAKIJUA KAMA WALINFANYIA
    MWAMBE. JOB YUSTINI YUPO KUWATETEA KITAELEWEKA HUKO 2025. CHAPENI KAZI ZIBENI MASKIO KWA WACHELEWESHAJI HAWA.

    MWINYI KA.. KAA PEMBENI. KINA MAMA WANATOSHA,, WACHA ROHO YA KOROSHO..!!!

    ReplyDelete

Top Post Ad