Harden aipiga chini ofa yenye rekodi kabambe NBA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


 Nyota wa Houston Rockets, James Harden amekataa ofa ya mkataba mpya wa kuendelea kusalia klabuni hapo kwa miaka miwili zaidi huku akifungua milango ya kujiunga na Brooklyn Nets kwa msimu ujao.


Ofa mpya aliyopewa MVP huyo ingemfanya aweke rekodi ya kuwa mchezaji pekee katika NBA kuchukua mshahara wa dola milioni hamsini ambazo ni zaidi na bilioni 116 za kitanzania.


Imearifiwa kwamba staa huyo ambaye ni MVP wa msimu juzi ameshawishika kuungana na Kevin Durrant na Kyrie Irvin akiamini utatu huo mtakatifu utawasaidi kutwaa taji la NBA.


Rockets ilimpoteza kocha wake Mike D'Antony na meneja mkuu Darly Morey baada ya kufungwa na mabingwa Los Angels Lakers katika mchezo wa nusu fainali wa kanda ya magharibi.


Harden aliungana na Russel Westbrook msimu uliopita akiamini watafanya makubwa katika timu yao lakini mambo yakawa tofauti.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad