google-site-verification: googleb0bc30c3e5fdb812.html Jiwe Kubwa la Almasi Lagunduliwa Botswana | UDAKU SPECIAL

Jiwe Kubwa la Almasi Lagunduliwa Botswana

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Moja kati ya mawe makubwa ya almasilimechimbwa nchini Botswana na mchimbaji mdogowa Canada, ambaye ameendelea kugundua mawe makubwa.

Kampuni ya Lucara Diamond Corp. imesema imebaini almasi nyeupe ya karati 998, na kufanya kuwa miongoni mwa mawe makubwa matano kuwahi kugunduliwa. Lucara amesema almasi hiyo itahitajika kuigawa vipande kabla ya kuisafisha.


Mgodi wa Karowe umekuwa maarufu kwa kugundua mawe makubwa. Mwaka 2015, kampuni iligundua jiwe la karati 1,109 Lesedi La Rona , lililouzwa kwa dola milioni 53, na pia jiwe la karati 813 lililoweka rekodi ya kuuzwa kwa dola za Marekani milioni 63.


Kwa mujibu wa gazeti la Bloomberg , Jiwe kubwa kabisa la almasi kuwahi kugunduliwa ni la karati 3,106 Cullinan, lililogunduliwa Nchini Afrika Kusini mwaka 1905.


Kwa mujibu wa Forbes Lucara, ambayo iliuza mawe yake mawili mwakubwa kwaLouis Vuitton , imesema inafanya tathimini hatua zinazofuata na mshirika wake wa shughuli za kukata na kusafisha HB Antwerp.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad