Mambo Yatakayokuepusha na Ugonjwa wa Kisukari

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Ugonjwa wa kisukari ni moja ya magonjwa yasiyoambukiza, ambayo husababishwa baada ya kongosho kushindwa kutengeneza 'insulin' ya kutosha ndani ya mwili.


Insulin ni homoni ambayo kazi yake kubwa ndani ya mwili ni kurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu.


Sasa leo naomba nikwambie wewe msomaji wangu haya mambo saba ambayo ukiyafanya kila siku unaweza kujiweka mbali na ugonjwa huu wa kisukari.


1. Kuwa na uzito wa kawaida

Zingatia kuwa na uzito unaoendana na wewe kiafya kwani hali ya uzito mkubwa huweza kuwa chanzo cha tatizo hili la kisukari. Unapokuwa na uzito wa kawaida unaambiwa kuwa utakuwa umejiweka mbali na ugonjwa wa kisukari kwa asilimia 6.


2. Zingatia ulaji bora

Unapaswa kula chakula kwa kufuata taratibu bora za kiafya ikiwa ni pamoja na kuzingatia ulaji wa matunda pamoja na mbogamboga.


3. Kunywa maji ya kutosha

Unashauriwa kunywa maji ya kutosha kadri uwezavyo, unatakiwa kunywa angalau glass 7 hadi 8 kwa kila siku


4. Usisahau kufanya mazoezi

Mazoezi ni muhimu kwa kila mtu, hivyo kama wewe unapenda kuepukana na ugonjwa huu wa kisukari ni vyema kujitahidi kunywa maji ya kutosha kila siku.


5. Epuka msongo wa mawazo

Mawazo nayo yanapozidi huweza kuwa chanzo cha tatizo hili la kisukari, hivyo jitahidi kuepuka tabia ya kuwa na msongo wa mawazo mara kwa mara ili kujiweka mbali zaidi na ugonjwa wa kisukari.


6. Pata muda wa kutosha wa kulala

Kulala nako ni muhimu kwa afya zetu wanadamu pia ni moja ya njia ya kufanya kuepuka na ugonjwa huu wa kisukari


7. Fanya uchunguzi wa afya mara kwa mara

Jitahidi kujenga utaratibu wa kuchunguza afya yako mara kwa mara ili iwe rahisi kugundua matatizo yako ya kiafya mapema kabla ya tatizo kuwa kubwa zaidi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad