Mbunge wa Chadema Pekee Aliyechaguliwa Asema Hatowasaliti Wananchi Waliomchagua..."Tutabanana Bungeni"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Aida Khenan, Mbunge Mteule wa Nkasi Kaskazini kupitia CHADEMA amesema, hatowasaliti wananchi waliomchagua hivyo atakwenda Bunge kuapishwa ili aweze kuwatumikia.


Aida ni Mgombea pekee wa Ubunge kupitia CHADEMA aliyetangazwa mshindi katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 28, akimshinda Ally Kessy wa CCM aliyekuwa anatetea jimbo hilo aliloongoza kwa miaka 10.


Kauli hiyo imekuja baada CHADEMA na ACT-Wazalendo kutangaza kutoyatambua matokeo ya Uchaguzi yaliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) hata kwenye maeneo waliyoshinda.


Katika Bunge lililopita, Aida alikuwa Mbunge wa Viti Maalum. Lakini sasa amesema yeye ni Mbunge ambaye anasubiri kuapishwa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad