Msumbiji yakana taarifa za raia kukatwa vichwa na wanamgambo wa Kiislamu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Serikali ya Msumbiji imekana ripoti kuwa kumekuwa watu wamekuwa wakikatwa vichwa na wanamgambo wa kiislamu katika mji wa Cabo Delgado.


Gavana wa eneo hilo lenye utajiri wa mafuta, Valige Tauabo, amesema kuwa hakuna matukio ya mauaji ya hivi karibuni katika wilaya yoyote ya mji huo, tofauti na ripoti zinavyoeleza.


Aliongeza kuwa ripoti ya mwisho ya mauaji yaliyotekelezwa na wanamgambo wa Kiislamu yalikuwa tarehe 6 mwezi Aprili.


Vyombo vya habari viliripoti kuwa zaidi ya watu 50 walikatwa vichwa na wanamgambokatika uwanja wa mpira wa miguu katika kijiji, wilaya ya Miudumbe.


Watu wenye silaha waliimba "Allahu Akbar" (Mungu ni Mkubwa), walifyatua risasi, na kuchoma moto makazi ya watu walipovamia kijiji cha Nanjaba, usiku wa Ijumaa, Shirika la habari la Msumbijililiwanukuu manusura wa tukio hilo.


Gavana Tauabo alisema kumekuwa na tu "uvamizi wa waovu" ambao walikuwa wakifuatiliwa na jeshi.


Aliongeza kuwa serikali inasikitishwa kuhusu kuenea kwa ghasia za silaha huko Cabo Delgado.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kwani Mtundu Bovu kam Ponda.? wapi yuko

    ReplyDelete

Top Post Ad