Mwanasheria nchini Nigeria ataka maandishi ya kiarabu kwenye fedha yaondolewe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mahakama mjini Lagos Nigeria inatarajia kusikiliza kesi iliyofunguliwa na mwanasheria dhidi ya Benki Kuu ya Nigeria akitaka kuondolewa kwa maandishi ya kiarabu kwenye fedha za nchi hiyo.

Malcolm Omirhobo pia anataka jeshi la Nigeria kuondoa maandishi kutoka kwenye nembo ya jeshi yanayoashiria kuwa Nigeria ni nchi ya Kiislamu, kinyume na katiba ya nchi hiyo kuwa ni taifa lisilofungamana na dini yoyote.


Mwanasheria huyo anataka maandishi hayo yawekwe kwa lugha ya Kiingereza au kwa lugha yoyote miongoni mwa lugha tatu zinazotumika nchini humo –Hausa, Yoruba au Igbo.


Hatahivyo, Benki Kuu imekana kuwa maandishi hayo ni ishara ya Uislamu.


Watu wengi nchini humo, hasa eneo la Kaskazini , huongea Kiarabu. Hata hivyo Kiingereza ni lugha kuu ya mawasiliano nchini humo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad