Rais Magufuli ala kiapo na kutoa ahadi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Rais mteule Dkt John Pombe Magufuli ameapishwa rasmi  kuwa Rais  wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania huku akiapa na kuahidi kuwatendea haki watu wote.

Magufuli  ameapishwa leo Novemba 5, jijini Dodoma pamoja na Makamu wake Samia Suluhu katika Uwanja wa Jamhuri na sherehe hiyo imehudhuriwa na Viongozi  kutoka nchi mbalimbali akiwemo Rais wa Uganda ,Yoweri Museveni.


Katika kiapo chake , Rais Magufuli ameapa kuitetea, kuilinda na kuhifadhi katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na kuahidi kutumika kwa uaminifu katika kazi zake za urais


Sherehe hii ya uapisho wa Rais Magufuli inampa tena nafasi nyingine ya kuiongoza Tanzania kwa muhula mwingine tena 2020- 2025 mara baada ya kupata ridhaa kwa watanzania.


Rais Magufuli alitangazwa kuwa Rais wa mteule wa Tanzania Oktoba 30 na Tume ya Taifa ya Uchaguzi mara baada ya kuongoza kwa kura 12, 516, 252 dhidi ya wapinzani wake 14.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hongera Baba, Allah akulinde na Mahasidi wa ndani na nje.

    ReplyDelete

Top Post Ad