Sababu za Prince Dube kupelekwa Afrika kusini

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Klabu ya Azam FC imethibitisha kuwa mshambuliaji wake Prince Dube amevunjika mkono, mshambuliaji huyo aliumia dakika ya 15 kwenye mchezo wa ligi kuu bara dhidi ya Yanga, na anatarajiwa kwenda Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.


 

Dube raia wa Zimbabwe ambaye ndio kinara wa ufungaji wa klabu ya Azam msimu huu akiwa na mabao 6, alipata majeraha hayo baada ya kudondoka vibaya alipokuwa anawania mpira wa juu dhidi ya beki wa Yanga Bakari Nondo Mwamnyeto.


Taarifa iliyotolewa na klabu ya Azam inasema mshambuliaji huyo amevunjika mfupa wa mbele wa mkono wake wa kushoto unaoitwa Ulnar, huu ni mfupa unaoanzia kwenye kiwiko na kushuka hadi kwenye kidole cha mwisho.


Pia taarifa hiyo imeweka wazi kuwa Dube Ataondoka nchini Siku ya Jumapili ya Novemba 29, 2020 kuelekea nchini Afrika Kusini kwa matibabu zaidi, katika Hospitali ya Vincent Pallotti iliyopo Cape Town, chini ya daktari bingwa wa mifupa Robert Nicolas.


Azam FC wamekuwa wakiitumia hospital hii kuwatibia wachezaji wao tangu mwaka 2011.


Na kipigo walichokipata Azam FC hapo jana kinakuwa ni cha 3 msimu huu, na sasa wameshuka mpaka nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi wakisalia na alama zao 25 ikiwa ni tofauti ya alama 3 dhidi ya vinara Yanga SC wenye alama 28.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad