"Sasa Young Lunya amevuka mipaka" - Nikki wa Pili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Msanii wa HipHop kutoka kampuni ya Weusi Nikki wa Pili amesema rapa Young Lunya ameweza kwenda mbele zaidi na kuvuka mipaka kwa kutumia 'digital platform' kwenye upande wa biashara kwa wasanii wanaochipukia.

 

"Msanii mchanga wa HipHop anapokuwa anaanza inabidi awe na mipaka ya kuvuka mbele mfano Whozu alitumia 'digital platform' kutoka, mpaka sasa Young Lunya ndiyo ameweza kuvuka mipaka kwa kutumia 'digital', ameenda mbele ya kuwaza kurap ili wengine wafikirie zaidi biashara ili waweze kupenya" 


Aidha Nikki wa Pili ameongeza kusema "Rap sio rahisi kuishika, wasanii wengi wa rap hawana uwezo au hawana watu wakuwasogeza mfano Young Lunya ametumia ujanja hata nyimbo zake zimebebwa kutokana na ubunifu wake"


Young Lunya ni msanii anayewakilisha kundi la OMG Tanzania na tayari ameshaachia kazi zake ambazo zimefanya vizuri kama tikisa kichwa, fimbo, moto, na freestyle session 1,2,3.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad